Namna ya kutajirika ukiwa Tanzania

 



Watanzania wengi wamekuwa wakitamani sana kukimbilia nchi za nje kwa ajili ya kutafuta maisha et Tanzania hakuna maisha.

Mimi napingana na mtazamo huu kabisa kwani Tanzania ina kila fursa ambazo unaweza usizipate katika nchi zingine. Watu wengi ambao wangezitumia fursa hizi wasingetamani kwenda ulaya kuishi kama watumwa kwa mabosi wa huko. 

Mfano mtu aliyetakiwa kusafirisha( export ) mazao Ulaya  anaenda ulaya kuzoa uchafu na kuosha magari eti sifa kwamba yupo Ulaya hii ni huzuni kubwa sana kwa Taifa. 

"I shall become millionaire in the same Tanzania people are running away to Europe "

Kuna fursa kuu mbili ambazo kama mtanzania akizitumia vizuri bila kisingizio cha viongozi wa serikali anaweza kuwa milionea ndani ya muda mfupi sana. Angalia hapa chini::




  1. Kilimo: Nchi nyingi duniani hapa Tanzania  ni mojawapo ya  nchi iliyo na aridhi kubwa sana na ambayo haijatumika.  Tanzania inaweza kulisha bara la Ulaya bila shida yoyote. Wakati Ulaya wanakuja kutafuta malighafi Tanzania halafu watanzania wanakimbilia Ulaya kutafuta maisha really this is sad. Ukijikita katika kilimo na kushirikisha wataalamu katika mipango yako ya kilimo rafiki yangu, yaani utatoboa vizuri mno kwani kila binadamu anahitaji kula.Kama biashara ya kudorora hapa duniani biashara ya chakula ndiyo itakuwa ya mwisho kudorora na wakati huo binadamu watakuwa wameisha duniani.
2. Ufugaji: Ufugaji unaweza kumtajirisha mtanzania kwa haraka sana kama atafuata ushauri wa wataalamu katika sector hii, na kufuata miongozo ya Sheria za nchi. Soko la nyama ni kubwa sana hapa Tanzania na nje ya Tanzania. Angalia tu kwa sasa nyama ilivyopanda bei,( nyama ya ng'ombe kwa mwanza ni 10,000 hii ni kawaida ,stek 13,000) kiuchumi maana yake mahitaji ni makubwa sana ya bidhaa hii. Sheria ya uchumi huwa bidhaa ikiwa adimu basi tegemea bei kupaa sana ndicho kinachotokea sasa  ila mtanzania anaangalia tu,anawaza ulaya. 

     Kwa sasa kuna soko kubwa sana la mbuzi Madagascar chukua point hiyo mtanzania mwenzangu.

Kama unahitaji ufafanuzi zaidi na ushauri wa kibiashara tafadhali wasiliana nami kama ifuatavyo;
Email; mkmconsultingservice@gmail.com 
Simu; +255 763 826 410
Website: www.makeconservices.com



Tunahitaji kuamka watanzania siyo wakati wakukaa kulaumu viongozi wa serikali bali ni wakati wa kukaa chini kutengeneza ramani ya hatima ya maisha yako 
Hatima ya maisha yako haipo mikoni mwa serikali.
Unapokuwa mtu mzima unawajibu wa kuchukua hatma mikononi mwako rafiki yangu.
Stay blessed 
By Lushinge Makelemo.
Business consultant.

Post a Comment

Previous Post Next Post