Ili kuwa na biashara kubwa si lazima uwe na mamilioni ya pesa kama mtaji,bali inategemea mifumo madhubuti unayoweza kuiweka kwenye biashara yako .
Watu wengi sana wameanza biashara na mitaji mikubwa lakini mwisho wa siku wameishia kufilisika na biashara zao kufa vibaya sana kwa kutozingatia mifumo mizuri ya uendeshaji wa biashara zao.
Unaweza kuanza na mtaji hata kuanzia 200,000 mpaka 500,000 ukawa millionaire kwa kufanya udhibiti kama wanaofanya wenye makampuni makubwa hapa duniani.
Mifumo ya kifedha [financial Management] ndo tiba pekee .Lazima uifanye biashara yako ni tofauti kabisa na wewe, chukulia kuwa ofisi yako au duka ni mtu mwingine kabisa.
Kosa kubwa wafanyabiashara wanalolifanya ni kuifanya biashara kama ndo yeye mwenyewe hivyo hujkuta akijisikia kuchukua kiasi cha pesa chochote anachota tu bila utaratibu. Tabia his husababisha kushindwa kutathimini mwenendo wa biashara yako .
Ukianzisha biashara hakikisha unaweka angalau 10% ya kila faida unayoipata katika biashara yako na hii pesa kamwe isiguswe mpaka itakapokuwa kiasi kikubwa kuweza kufungua biashara nyingine au kupanua biashara iliyopo.
Jitahidi kufanya mahesabu kila wiki au kila mwezi na kufanya ulinganifu na kuweza kuchukua hatua stahiki kunapokuwa na changamoto yoyote katika biashara yako. Pia uweze kujua faida na hasara unayoipata, na kufanya marekebisho panapohitajika.
Pia kama una mtaji wako mwenyewe usiingiwe na tamaa ya kwenda kukopa pesa kuongeza kwenye biashara yako, maana tatizo la kuanza biashara kwa mkopo haitaweza kukua kwa wakati au yaweza kufa ndani ya muda mfupi sana.
Nimeona watu wengi sana wakianzisha biashara zao kwa mikopo wameishia kufilisika na kupata aibu kubwa kwenye Jamii. Mtu anapokopa ili kuanzisha biashara hatakuwa na utulivu katika biashara yake, atakuwa hawazi kukuza biashara bali anawaza marejesho ya mkopo tu.
Tena siku hizi kuna aina ya mikopo wanaiita kausha damu, watu hawa wana riba kubwa sana na unatakiwa kila siku au kila wiki upeleke rejesho je hapo ndugu yangu utatoboa kweli?
Kuna mtu mmoja mkoa fulani hapa Tanzania anafanya biashara hizi za kukopesha ukichukua 100,000/= kila siku inazaa 10,000/= sasa niambie katika Hali huyo utafaulu? La hasha si rahisi
Ushauri wangu; Anza na kidogo ulichonacho kikuze taratibu bila haraka mwisho utakuwa mfanyabiashara mkubwa sana bila stress.
Hakuna raha kubwa duniani ukiishi bila kudaiwa .
Kwa Ushauri zaidi wa kibiashara na fedha wasiliana nasi;
0763 826 410
Lushinge Makelemo
EMAIL: lmakelemo@yahoo.com
mkmconsultingservice@gmail.com
Tags:
Pictures